UTAFANYA NINI BAADA YA MAISHA HAYA YA KAZI YA KULIELIMISHA TAIFA?
- JE,UTAOMBA TENA MKATABA WA KAZI?
- UTASALIA NYUMBANI TU?
- UTAANZA KUNUNUA NYUMBA YA KUISHI?
- UTAKUWA TEGEMEZI KWA WANAO?
- UTAFANYA BIASHARA?
LEO MIMI NAKUSHAURI UANZA KUJIFUNZA "BIASHARA" ILI IANZA KUKUZOEA KABLA HUJASTAAFU MWALIMU WANGU!!
BIASHARA SI MTAJI PEKEE BALI NI "KUTHUBUTU" BASI NAKUSII ANZA LEO KUTHUBUTU KABLA HATA HUJASTAAFU MUNGU AKIKUJALIA.UTAKAPO KUWA TAYARI NDANI YA BIASHARA ITAKUWA RAHISI KWAKO KUTUMIA KAKIINUA MGONGO KATIKA KUIMARISHA BIASHARA YAKO TU BADALA YA KUSUBIRI MPAKA UNASTAAFU NDIPO UANZA MARA - NYUMBA, BIASHARA MASHAMBA N.K.
BASI LEO NIKUPATIE VIONJO VYA NAMNA YA KUFANYA BIASHARA ANGALAU NDOGO:-MAMBO 7 YA KUZINGATIA KATIKA BIASHARA:-
1.THAMINISHA BIASHARA YAKO:
Iwe biashara kubwa au ndogo kumbuka bidhaa unazouza ni muhimu ziwe zenye ubora na mwonekano mzuri unaovutia wateja.("Good business man serves quality products to his customers")
2. PATA USHAURI KWA WATU WALIOFANIKIWA KI-BIASHARA:
Unapopata utata katika kufanya maamuzi sahihi ya nama ya kuanza biashara ni vizuri utafute ushauri kutoka kwa watu ambao tayari wamefanikiwa katika biashara kama yako.
3.FANYA BIASHARA YA KIPEKEE:
Kuwa mbunifu katika kubuni na kuibua aina ya biashara
4.UZA BIDHAA KWA BEI INAYOKUBALIKA NA WENGI:
Hapa haina maana uuze kwa bei poa bali uza kwa bei ambayo wengi wanaweza kuimudu.
5.TANGAZA BIASHARA YAKO:
Biashara ni matangazo hivyo huna budi kuitangaza redioni,runinga,magazeti,vipeperushi,mabango n.k.
6.JIAMINI NA USIKATE TAMAA KATIKA BIASHARA:
Kuna wakati na hasa unaponza biashara mambo huwa mabaya na hivyo ukaanza kukata tamaa,ni vyema ukajiamini na kutafakari na kujua ni wapi ulikosea na nini cha kufanya ili uboreshe biashara yako.
7.FANYA BIASHARA UIPENDAYO:
Naamini mtu ukiifanya kazi uipendayo utaifanya kwa uhodari na kupata mafanikio!
<<<<<"BIASHARA NI WATU"!!>>>>>
=====Na Mwalimu Mzoefu Darasani====!!
>> Huu ni ushauri wa bure....kwani mwisho wa maisha yetu ya ualimu tunaujua sisi wenyewe>>....!!