Saturday, June 14, 2014

LEO - NA - MWALIMU MZOEFU DARASANI

<>
Unaweza ukasoma sana lakini maisha yako yakawa ya wastani tu,unaweza usiwe na elimu lakini ukawa a maisha mazuri.Lakini kumbuka watu wote duniani wameendelea kutokana na elimu na ndiyo maana elimu inasisitizwa.Sasa hihi nini maana yake?
  Maana yake ni kwamba, "MAISHA MAZURI UNAWEZA KUYAPATA HATA KAMA HUNA ELIMU" Sasa kitaalamu sisi walimu tunasema hivi "ELIMU NI MUHIMU KATIKA KUENDELEA KUWA NA MAISHA MAZURI"
   Kitu muhimu hapa ni kule KUENDELEA kuwa na maisha mazuri ndiko kunakohitaji elimu,na ndo maana tunahitaji elimu kwa kila jambo kwa lengo la kuendelea kuwa na maisha mazuri kwa maana hiyo,ukiwa na elimu toka mwanzo wa kutafuta maisha yako ni bora zaidi-kwani utakuwa umejijengea maisha bora na ENDELEVU.....!
........Ni ushauri tu ....Na Mwalimu Mzoefu Darasani"!!

LEO - NA - MWALIMU MZOEFU DARASANI

"LEO - NA - MWALIMU MZOEFU DARASANI"

LEO-- NA - MWZOEFU DARASANI>>>!!!

Monday, June 9, 2014

Kawaida waakati wa likizo ni wakati wa mwanafunzi kupumzika na kumsaidia mazazi kazi ndogondogo za nyumbani,na wengine kwenda kuwatembelea ndugu na jamaa.Lakini baadhi ya wazazi wanawageuza watoto wa shule vitendea kazi kwa kufanya biashara ndogondogo eti ndiyo staili ya kumsaidia mzazi.
   Suala kipato cha familia ni jukumu la wewe mzazi na si vinginevyo mtoto wakati wake bado mwache apumzike na kujisomea----Msitulaumu walimu tu...."ELIMU YA MTOTO WAKO HUANZIA NYUMBANI" Mwalimu ni msaada tu

Friday, June 6, 2014

ELIMU...ZAIDI YA ELIMU...!!!

Busara huhitajika hata kama una elimu yako
SIKU HIZI ZA KARIBUNI UMEWAHI KUSHUHUDIA NA UNAENDELEA KUSHUHUDIA:

  • WATU WANAVAA VIZURI
  • WATU WANAVAA NUSU UCHI
  • WATU WANAPIGA PICHA ZENYE UBORA WA HALI YA JUU
  • WATU WANAPIGA PICHA ZA UTUPU
  • WATU WANAONGEA KIINGEREZA KIZURI
  • WATU WANAONGEA KISWA-NGLISH
  • WATU WANAINGIA KATIKA SIASA KWA WINGI
  • WATU WANACHANGIA VURUGU/MTAFARUKU BUNGENI
  • WATU WANAANZISHA SHULE ZA UHAKIKA
  • WATU WANAANZISHA SHULE KAMA UYOGA MAHALI POPOTE
  • NA MENGINE MENGI YANAYOFANANA NA HAYO!!
UNAJUA SABABU YA HAYA YOTE?
      Watu wamefika mahali na kuonekana hakuna asiyesoma hapa Tanzania.....na kwa maana hiyo kuonekana aliyesoma ni kama hajasoma na asiyesoma ni kama ana elimu zaidi ya elimu....na kwa kukuhakikishia kuwa yeye ameelimika basi anafungua na mitandao na kuiga kila kitu anachokiona humo-Matokeo yake,na yule aliyesoma kiuhakika ili asipitwe na huyo mpumbavu-mwenye elimu zaidi ya elimu basi naye anajiingiza katika mkumbo huo wa kuiga kila kitu ili amshshinde yule mwenye elimu zaidi ya elimu.
      Ndiyo maana leo hii mitandaoni utashuhudia:

  • WASOMI NA WASIO WASOMI
  • MAARUFU NA WASIO MAARUFU
  • WANASIASA NA WASIO WANASIASA
  • VIONGOZI NA WASIO VIONGOZI
  • WALIMU NA WASIO WALIMU
  • WANAFUNZI NA WASIO WANAFUNZI
  • WALEMBO NA WASIO WALEMBO
  • WASANII NA WASIO WASANII
  • WATANGAZAJI NA WASIO WATANGAZAJI
  • NA WENGINE KAMA HAO
Wakifanya vituko vinavyowashangaza watanzania kila kukicha --utashuhudia katika:

  • RUNINGA
  • REDIO
  • MAGAZETI
  • MITANDAO
  • SIMU-UJUMBE MFUPI
N/B:-MWALIMU -  MZOEFU DARASANI - NASEMA HIVI:
         "WATU SIKU HIZI WANASOMA SANA LAKINI HAWAELIMIKI"- HILI NDILO TATIZO
           TULILONALO KWA SASA!
Huu ni mtazamo wangu tu>>>> Kama Mwalimu Mzoefu Darasani>>>!!
Uzoefu unaonesha,elimu huanzia nyumbani kwa     baba na mama-mwalimu anafuatia tu!


Tuesday, June 3, 2014

aka A-One
Achana na katiba na mambo yake,achana na ukawa na mambo yake,achana na ahadi za kupanda kwa kima cha chini cha mishahara mimi nazungumzia namna gani mwanafunzi anavyoweza kufaulu mtihani wake wa mwisho:
          1.Ajiandae vizuri katika mitihani yake ya majaribio k.v.mitihani ngazi ya shule,kata,wilaya na mkoa.
       2.Kila siku ahudhuriapo shuleni ajiwekee ratiba yake binafsi k.m,leo nitasoma somo fulani
       3.Ashirikiane na wenzake kupata kile ambacho yeye hana.
       4.Aombe msaada kwa mwalimu wake pale tu darasa zima linapokosa jibu kwa swali lake.
         Ni ushauri tu..........kwa wanafunzi na walimu wenzangu wanaofundisha darasani>>>>>!!
                         Na mwalimu mzoefu darasani .....!!! 
Mwl Mzoefu.

achana na katiba na mambo yake,achana na ukawa na mambo yake,achana na ahadi za kupanda kwa kima cha chini cha mishahara mimi nazungumzia